SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Friday, January 21, 2011

LYOD NCHUNGA AZUNGUMZIA MATATIZO YAKE NA WANAYANGA NDANI YA KLABU HIYO.!!!


Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga Lyod Nchunga akiongea na wanahabari leo kwenye makao makuu ya klabu hiyo wakati alipotoa tamko la kulaani mkutano ulioitishwa na wanachama wa Yanga jana Klabuni hapo na kumtaka ajiuzulu kwa kukiuka katiba ya Klabu hiyo.
Nchunga amesema mkutano huo ulikuwa batili na ni uvunjaji mkubwa wa katiba ya Yanga lakini akaongeza kwamba watu wana hofu na msimamo wake wa kuamua kufanya ukaguzi wa mahesabu ya klabu hiyo kitu ambacho kinawatisha watu ambao wamekuwa wakitumia vibaya fedha za klabu hiyo.
Kikao hicho kilimtuhumu Nchunga kwamba amemuandikia barua Ndg Francis Kifukwe ili aandae mchakato wa kampuni ya biashara ambayo itaanza kuuza vifaa vya michezo vya Klabu hiyo. Lyod amekiri kukiuka utaratibu kwa kuandika barua hiyo na amesema hajapokea barua yeyote ya kumpa adhabu lakini kama watamuandikia barua hiyo ataipokea na kujua hatua gani atachukua.
Aliyepo Kulia katika picha ni Katibu mkuu wa Klabu ya Yanga Lawrence Mwalusako.

No comments:

Post a Comment