SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Friday, December 31, 2010

MH.UMMY ATEMBELEA TUJIKOMBOE GROUP TANGA!!!


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Bi.Ummy Ally Mwalimu kulia akipokea risala kutoka kwa Mwasisi Mshauri wa Shirika lisilo la kiserikali la Tujikomboe Group Bw.Shamsi Mhina ,Shirika hilo lenye makao yake Ngamiani Kusini Tanga linalojishughulisha na masuala ya kutetea haki za watoto,Maendeleo ya Jamii(Picha na Benedict Kaguo)

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Bi.Ummy Ally Mwalimu (katikati asiye na kilemba) akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Tujikomboe Group alipowatembelea jana,kulia ni Bw.Shamshi Mhina Mwasisi na Mshauri wa Shirika hilo,kushoto ni Bi Chiku Athumani Mratibu wa Shirika hilo Tanga,walioko nyuma ni Afisa Tawala Bi.Mariam Amiri na Mwanaisha Issa Msaidizi wa Ofisi,Naibu Waziri alitembelea kujua shughuli za asasi hiyo(Picha na Benedict Kaguo)

Thursday, December 23, 2010

WADAU NAWATAKIA SIKUU NJEMA YA X-MASS !! NITAKUWA KIMYA KIDOGO MPAKA BAADA YA X-MASS!!


Mimi Director wa Blog (Pashua)hii ya Eazymen nawatakia wadau wote Heri na fanaka katika kusherehekea sikukuu ya X-Mass.
Nitakuwa kimya mpaka baada ya sikuu kwa hiyo wadau tuwiane radhi.

PROF,NDULU PRESENTED THE TANZANIAN SHILING CURRENCY NOTE TO PRESIDENT KIKWETE TODAY!!!


The Governor of Bank of Tanzania Prof.Benno Ndulu today presented the new Tanzanian shilling currency note to President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete at Dar es Salaam State House this afternoon. The New Currency Note will be in circulation from January next year and they will be used alongside with the current bank notes. In the Picture The Central Bank Governor(left) Prof.Benno Ndulu presents a special album with new Tanzanian shilling currency notes to President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete while the Minister for Finance Dr.Mustafa Mkullo,(right) looks on.

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete examines special security features in some of the new banknotes presented to him by the Governor of the Central Bank Prof. Benno Ndulu at Dar es Salaam State House this evening.

A senior Principal bank Officer, from the Central Bank’s Directorate of Banking, Mr.Juma Hassan Kimwaga shows President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete, special security features in the new Tanzanian shilling currency notes at Dar es Salaam State House this evening.(photos by Freddy Maro).

TID KUZINDUA ALBUM YA SIFAI DESEMBA 28,2010.CLUB BILLICANAS!!

WAZIRI NUNDU AWASHUKIA WATENDAJI TPA WANAOTAKA UTAJIRI WA HARAKAHARAKA KWA NJIA YA RUSHWA!!!


Waziri wa uchukuzi Omari Rashid Nundu (kushoto)na Naibu wa waziri wa wizara hiyo Mhandisi Athumani Mfutakamba(wa pili kushoto),wakimsikiliza kwa makini meneja wa kitengo cha kuhudumia makontena bandarini(TICTS),Donald Talawa(kulia)akiwaeleza namna kitengo hicho kinavyofanya kazi zake,alipotembelea kituo cha kitengo hicho kilichopo Ubungo jijini Daresalaam.

Waziri wa uchukuzi Omari Rashidi Nundu (kushoto)akikagua kituo cha kuhudumia makontena cha kampuni ya AMI,alipofanya ziara ya kukagua shughuli zinazohusiana na mamlaka ya bandari Tanzania (TPA)jijini Daresalaam.wapili ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo Grant Lendrum.

Mawakala wa kutoa magari bandarini wakitoa madukuduku yao mbele ya waziri Nundu wakati wa ziara hiyo.

Sunday, December 19, 2010

RATIBA YA MAZISHI YA NGULI WA DRUMS ABUU SEMHANDO,BABA DIANA !!!


Waliosimama..Remmy Ongala, Abuu Semhando, Kasaloo Kyanga, Fan Fan

Ratiba ya Mazishi ya mwanamuziki na na meneja wa Bendi ya African Stars-Twanga Pepeta Marehemu Abou Ally Semhando “Baba Diana”
· Jumamosi ndugu na jamaa walikusanyika nyumbani kwa marehemu, Mwananyamala Kisiwani(Ngilangwa) kwa ajili ya kutoa pole na kuwafariji wafiwa.

· Leo Jumapili 19/12-Saa11 baada ya Swala ya alfajiri katika msikiti wa Muhimbili, waombolezaji kuingia katika magari na kuelekea kijiji cha Kibanda, Muheza tayari kwa mazishi.

· Mara baada ya chakula cha mchana mwili kupelekwa msikiti wa Muheza nabaada ya swala mwili kupelekwa makaburini kwa maziko.

· Waombolezaji watarejea Dar es Salaam baada ya maziko.

Hakika Msiba wa Abou unaumiza sana

1. Jumamosi ni siku aliyokuwa amuoze binti yake wa kwanza
2. Alikuwa ameuandikia uongozi wa Bendi kuwa umpe likizo ya mwezi kwani alitaka asiweko katika jukwaa kwa kipindi. Ni mara ya kwanza yeye kuandika barua ya kuomba likizo
3. Katika simu yake ringtone aliyoiweka ni ya wimbo wa Njohole Jazz Band- bendi hii wanamuziki wake karibu wote walikufa pamoja katika ajali mbaya ya gari.


4. Alikuwa mpiga drum wa Dk. Remmy Ongala enzi za Super Matimila na mtindo wao wa Talakaka mwaka 1981

-John Kitime

Tuesday, December 7, 2010

PETER MSECHU AMBAYE NI MSHINDI WA PILI TUSKER PROJECT FAME4 AWASILI JIJINI DAR LEO MCHANA NA KUPOKEWA KWA SHANGWE !!!


Mshindi wa pili wa Tusker project fame4 kutoka Tanzania Peter Msechu akiwapungia mkono baadhi ya mashabiki wake waliojitokeza kumpokea katika uwanja wa ndege wa mwalimu Nyerere Dar leo mchana.

Peter Msechu akiwa na mchumba wake anayeitwa Amalis katika picha ya Pozi.

Blog hii ya Esymen pamoja na studio ya muziki ya blog hii ijulikanayo kama 2MORROW RECORDZ iliyopo jijini Tanga ambapo tuliwahi kufanya baadhi ya kazi pamoja na wewe tunakupongeza kwa ushindi huo ulioupata.

Friday, December 3, 2010

MH UMMY MWALIMU AANZA KAZI KWA KUWA MGENI RASMI SHEREHE ZA WALEMAVU !!!


Mhe. Ummy Ali Mwalimu akimkabidhi Mtoto mwenye Ulemavu wa Miguu Baiskeli ya kumwezesha kutembea.Hii ilikuwa ni wakati wa Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu iliyoadhimishwa kitaifa huko Mkuranga. Jumla ya Baiskeli 50 Zimetolewa kwa Ajili ya kuwasaidia Watu wenye Ulemavu Wilayani humo.

Mhe.Ummy Ali Mwalimu akisoma Hotuba yake wakati
Siku hii ya Walemavu huko Mkuranga.


Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii, wanawake na watoto, Mhe.Ummy Ali Mwalimu,Mhe.Al-Shymaar wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Henry Orauya( Kulia) pamoja na Viongozi Wakuu wa Wilaya hiyo, mara baada ya kuwasili Wilayani hapo.
Sisi wananchi wenzako wa Tanga tunajivunia kwa Mh Raisi kukuchagua kuwa Naibu waziri na tunakutakia kila la heri katika kazi zako za Unaibu Waziri na katu usiutupe mkoa wako wa Tanga.Tanga Oyee!!!:-)

Thursday, December 2, 2010

WAZIRI MAGUFULI AMTIMUA KAZI CEO WA TANROADS !!


Waziri wa ujenzi Dk John Magufuli ameanza kazi kwa maamuzi magumu kwa kumfukuza kazi mtendaji mkuu(CEO)wa wakala wa barabara Tanzania(TANROAD)Ndg Ephraim Mrema.
Habari za uhakika ambazo Nipashe limezipata kutoka vyanzo vya kuaminika zianaeleza kwamba Magufuli alifanya uamuzi huo jana.
Vyanzo hivyo havikueleza sababu ya kumtimua mrema zaidi ya kusema uamuzi huo unaanza mara moja.
Habari zaidi zinasema kuwa Dk Magufuli alimtaka Mrema kukabidhi ofisi jana mchana na nafasi yake inashikiliwa kwa muda na mkurugenzi wa barabara za vijijini Patrik Mfugale.
Hata hivyo Nipashe lilimtafuta Dk Magufuli jana usiku ili kuthibisha uamuzi huo lakini simu yake ya kiganjani ilikuwa imezimwa.habari kwa hisani ya nipashe.

Wednesday, December 1, 2010

DR GHARIB BILAL AADHIMISHA SIKU YA UKIMWI KITAIFA MKOANI MOROGORO !!!


Makamu wa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Ghalib Bila,akikabidhi cheti na kikombe kwa muwakilishi wa shirika la champion kwa ushiriki wake bora katika maonesho ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyoadhimishwa kitaifa mkoani Morogoro leo.

wasanii wa kundi la vichekesho la Orijino komedi wakiwaburudisha wananchi wa mkoa wa Morogoro waliohudhuria maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri.

Makamu wa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Mohamed Ghalib Bilali akilihutubia taifa kwenye maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika kitaifa katika uwanja wa jamhuri mkoani Morogoro.

Saturday, November 27, 2010

MWALIKO WA SHEREHE ZA UHURU WA TANZANIA NCHINI NORWAY!!!


WATANZANI WAISHIO BERGEN NORWAY TUNAFUNGUA UMOJA WETU WA WATANZANIA HAPA BERGEN NA PAMOJA NA KUSHEHEREKEA SIKU YA UHURU WA TANZANIA KWA PAMAMOJA NA WATANZANIA WENZETU POPOTE WALIPO DUNIANI SIKU YA TAREHE 10.12.2010.

KATIKA SHUGHULI YETU HII MGENI RASMI ATAKUA NI MWAKILISHI WA BALOZI WA TANZANIA KUTOKA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI SWEEDEN. TUNAWAKARISHA WATANZANIA WOTE WAISHIO BERGEN NORWAY NA NJE YA NCHI YA NORWAY KUJA KUJUMUIKA NASI KATIKA GHAFLA HII. NAWE UKIWA MMOJA WAPO KARIBU SAANA.

NAPIA TUNA PAGE YETU YA CHAMA KWENYE FACEBOOK INATAMBULIKA KWA JINA LA (WATANZANIA BERGEN) WATU WOTE WANAKARIBISHWA KUWA NA URAFIKI NASI, NA PIA TUNAKARIBISHA MAONI KWA KUPITIA ANUANU PEPE YA CHAMA NAYO NI ( WATANZANIA.BERGEN@GMAIL.COM)

UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.


KARIBUNI

Saturday, November 20, 2010

MDAU IDD AKISHOW LOVE NDANI YA BLOG !!!


Mdau wa Blog hii Ndg Idd ambaye anapatikana maeneo ya Hotnet street Tanga ,akishow love ndani ya Pozi la ukweli.

RAIS KIKWETE ASAKATA RHUMBA NA LYATONGA MREMA !!


JK akicheza na Mwenyekiti wa TLP na Mbunge wa Vunjo Mh. Augustine Lyatonga Mrema wakati wa mnuso wa kuwapongeza wabunge kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma. Kulia ni Mzee Yusuf ambaye kundi lake la Jahazi Modern Taarab lilikuwa likitumbuiza.
Picha na mdau Freddy Maro.

Wednesday, November 3, 2010

SAMWEL SITTA ACHUKUA TENA FOMU KUTETEA KITI CHAKE CHA USPIKA BUNGE LIJALO !!!


Spika anayemaliza mda wake Mhe. Samuel Sitta leo amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Uspika wa Bunge katika Bunge la Kumi kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mapema wiki ijayo mjini Dodoma.


Spika Sitta amechukua fomu hiyo kupitia chama chake cha CCM katika ofisi ndogo za CCM Lumumba, Dar es Salaam na kuijaza kisha kuirudisha leo hii baada ya kukamilisha mahitaji yote ikiwa ni pamoja na kugharamia fomu hiyo kwa kiasi cha Tsh 500,000/= kwa mujibu wa taratibu wa chama hicho.


kwa Mujibu wa ibara ya 84 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, chama chochote cha siasa kilichosajiliwa kina haki ya kushiriki katika Uchaguzi wa Spika kwa kumpendekeza mwananchama wake mmoja ambaye ni Mbunge au asiye Mbunge mwenye sifa za kuwa Mbunge kuwa Mgombea wa nafasi hiyo.



Katika picha juu Spika anayemaliza muda wake Mhe. Samuel Sitta akisaini kitabu cha watu waliochukua fomu ya kugombea nafasi ya Uspika kwenye Ofisi za CCM Lumumba.

RAIS MPYA WA ZANZIBAR DR SHEIN ALA KIAPO TAYARI KUONGOZA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA !!!


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe, Dk Ali Mohammed Shein Akila Kiapo cha kuwa Rais wa awamu ya saba wa Zanzibar katika sherehe zilizofanyika Uwanja wa Amaan Mjini Unguja leo.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe, Dk Ali Mohammd Shein, akikagua gwaride rasmi la vikosi vya ulinzi katika sherhe maalum cha kua kiapo cha kuwa Rais wa Awamu ya saba wa Zanzibar, katika uwanja wa Amaan Studiam, Mjini Unguja leo.

Tuesday, November 2, 2010

MWANAMUZIKI MR II (SUGU) SASA NI MHESHIMIWA JOSEPH MBILINYI !!!!


Mwanamuziki mkongwe na muanzilishi wa muziki wa Kizazi kipya maarufu kama Bongofleva nchini Tanzania MR II maarufu kama Sugu ameweza kushinda kwa kishindo nafasi ya Ubunge kwa jimbo la Mbeya Mjini kwa Tiketi ya Chama cha CHEDEMA.Mr II au Sugu amewashukuru watanzania hususani wakazi wa Mbeya Mjini kwa imani walioionyesha kwake kwa kumchagua kwa ushindi mkubwa kuwa mbunge wao kwa kipindi cha miaka 5 ijayo.Katika shukrani zake Sugu amewaahidi wakazi wa Mbeya mabadiliko ya ukweli ya kuleta maendeleo katika Jimbo hilo.

MRISHO MPOTO ASEMA WASANII WA TANZANIA WANA ULIMBUKENI WA KUIGA UTAMADUNI WA MAGHARIBI KWA KILA KITU !!!!


Mrisho Mpoto

Msanii mahiri wa mashairi nchini,Mrisho Mpoto ameeleza kile anachoamini kwamba,tasnia ya sanaa na wasanii wa Bongo hawawezi kamwe kupata mafanikio katika ngazi ya kimataifa kutokana na ulimbukeni wa kuiga sanaa za watu wengine, kudharau asili yao na kujipachika usupastaa wa kubumba.

Mpoto aliyasema hayo wakati akiwasilisha mada yake iliyohusu Muziki wa Asili na Mashairi kwenye Jukwaa la Sanaa Jumatatu hii ambapo alisisitiza kwamba,wasanii wa bongo wamekuwa ni wa kulalama na kulia njaa kutokana na kazi wanazozalisha kushindwa kabisa kupata mvuto wa kimataifa na kushindana kwani zimekuwa kwa asilimia kubwa zikifanana na tamaduni za nje hivyo kukosa jipya.

Akijitolea mfano yeye mwenyewe Mpoto alisema kwamba, ameweza kukaa chini na kubuni sanaa ya asili ya Tanzania ambapo amekuwa akighani mashairi na kuyaweka kwenye mdundo wa muziki na hivyo kupendwa na idadi kubwa ya watanzania na kupenya kimataifa hivyo kumfanya kupata mialiko na fursa nyingi za fedha ambazo zimekuwa zikimpatia mafanikio makubwa.

Kwake yeye Mpoto anaamini kwamba, Sanaa ya Tanzania na wasanii wake hawaonekani kugundua siri ya kufanya kazi za sanaa zenye asili yao na badala yake wamekuwa makasuku wa kujifananisha na kuishi maisha kama ya Ulaya na Marekani huku kazi zao zikifanana kila kitu na hizo za nje hali ambayo imeifanya sanaa kupwaya na wasanii wenyewe kuishi maisha ya njaa.

Aliongeza kwamba, ni ngumu kupata msanii wa bongo anayefanya sanaa peke yake kwani mara nyingi lazima wachanganye na shughuli zingine ili kupata kipato kutokana na kazi zao kutowalipa.Katika hili Mpoto anaamini kwa kiasi kikubwa limesababishwa na wasanii wenyewe kukosa ubunifu, kuiga kila kitu kutoka nje, kulewa sifa za mapema, kukumbatia sanaa zisizo za asili yao na kujipachika usupastaa wa kubumba.

“Nimekuwa nikipata mialiko mingi nje ya nchi,siku chache zijazo nitaenda Denmark,Finland,Ufaransa, na Uholanzi.Si kwa kuwa napendwa sana bali ni aina ya sanaa ninayofanya ina asili yangu ya Tanzania na inanitambulisha kila ninakokwenda.Waache wasanii wengine wavae nguo chini ya makalio yao au hata watembee uchi mimi nitabaki na magunia yangu.Hili ndilo naamini litaweza kunipa mafanikio na ninayapata” alisisitiza Mpoto.

Mpoto ambaye kwa sasa ni msanii pekee aliyepata mafanikio makubwa kutokana na kupata mikataba mingi ya matangazo, mauzo ya kazi zake na mialiko ya kimataifa kutokana na kukumbatia sanaa ya asili aliwashauri wasanii wa bongo kuacha kunakiri (kukopi) sanaa za nje na badala yake wakune vichwa katika kubeba sanaa ya asili ambayo hapana shaka itawatambulisha kimataifa na kuwapa mikataba minono ya ndani na ya nje.

Mpoto aliyekuwa ameambatana na muimbaji wake wa Mjomba Band,Ismail alisema kwamba, inatia aibu na kinyaa unapoangalia sanaa za bongo kwani zinaonekana kuandaliwa na watu wenye njaa, wanaosaka fedha za fastafasta kuliko kujali nini wanapeleka sokoni hali ambayo imekuwa ikiwafanya wasanii wa Tanzania waonekane ni wa hovyohovyo, wa kudharaulika na wasio na mkakati wa kufikia mafanikio ya kisanaa.

“Kuna watu wamefanya sanaa miaka nenda miaka rudi lakini hawapigi hatua.Wamekuwa ni watu wa kulalamika bila kuzingatia ni kwa kiwango gani sanaa zao zina ubunifu na kubeba asili na utambulisho wao.Ndugu zangu tusipozingatia haya mafaniko tutayasikia tu na tutakuwa watu wa kuganga njaa na kupiga mizinga ya vocha” alimalizia Mpoto

Thursday, October 28, 2010

THE AFRICAN ARTISTS HAVE REPRESENTED TO THE FULLEST ROCKSTAR 4000 !!!


8 SUPERSTARS FROM ACROSS AFRICA UNITE WITH ONE MAJOR GLOBAL MEGASTAR TO FORM ONE8 – THE ALL STAR GROUP TO TAKE THE BEST IN MUSIC FROM AFRICA ONTO THE GLOBAL STAGE, CONNECTING MILLIONS OF FANS THROUGH THE UNIVERSAL LANGUAGE OF MUSIC!


The wait is over and a revolution in music has officially begun! After weeks of speculation ONE8 is here!


Through the power of the universal language of MUSIC and combining genres, sounds, voices and audiences - while breaking down stereotypes, geographical borders and divisions, ONE8 is the ultimate music force that is single-handedly changing the face of the African music industry.


Planet music is the playground for ONE8 as the hottest African talent from eight major African countries has joined forces to create an African supergroup unlike anything seen before.


In fact the power of this collective of African stars and excitement has gotten so big that ONE8 will be not only be joined by one of the biggest global megastars and icons in music for their first single and video, about to be recorded in Chicago, USA but this superstar, who’s played a crucial role in defining R&B and Hip-Hop as we know it today around the world, will in addition produce the song and video together with some of the biggest names in music and music video production in the world today!


This all star group ONE8 is produced and managed by the first major Pan- African record label and 360 music company, ROCKSTAR4000 within the family of the world’s number 1 recording company Sony Music, who’s delivered the world some of the biggest icons and pioneers and boasting a vast catalog of some of the most important recordings in the history of music including the likes of Elvis Presley, Michael Jackson, Beyonce, R Kelly, Alicia Keys, Usher, Christina Aguilera, Pink, Neil Diamond, Bruce Springsteen, Santana, Shakira, Kings of Leon to name a few. ONE8 is destined for greatness shattering perceptions about African music as it builds networks and excitement across the Pan African music landscape and across the world.


ONE8 is not only just another big star group, but is a very progressive and digital media driven group, and hugely driven by their passion to not only allow their fans access around the clock but freedom from every day challenges and empowering their fans to be whatever they want to be through the power of music and the digital world - connecting them across cities, borders and continents. As all 8 artists set off for the USA, fans will be connected with them around the clock through the website, mobile site or mobisite, Facebook, Twitter, Flickr and YouTube and live webcasts from location and empower millions of fans to feel free to experience this music revolution and historic journey as it happens.

Fans will experience their favorite stars up close and personal and roam where no fan has roamed before, digital ALL ACCESS PASSES delivered personally by these superstars to their fans! Together all the artists have worked together to create a song that is a truly Pan-African creation. The group will also shoot a video in Chicago which will be released across the continent and the world with the first single in November, alongside a full album and DVD soon after.

Sunday, October 24, 2010

DR WILBROAD SLAA ATIKISA JIJI LA TANGA !!!!


Dr Slaa akiwahutubia maelfu ya wakazi wa jijini Tanga, muda mchache kabla hajakwenda Dar Es Salaam kwenye mdahalo.


Pichani Umati mkubwa wa wakazi wa Jiji la Tanga Ukimsikiliza Dr Wilbroad Slaa katika Viwanja vya Tangamano.

MWANAMUZIKI ALLY KIBA AZIDI KUNG'AA KIMATAIFA


Ali Kiba Kusepa Marekani, kupiga kolabo na R.Kelly
-------

Kutoka ndani ya mradi wa muziki wa kizazi kipya, msanii Ali Kiba anatarajia kuondoka leo kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya kugonga ngoma ya pamoja na baadhi ya mastaa wa Afrika, kabla ya kufanya kolabo na staa wa kimataifa, Robert Kelly wa pande hizo.

Kwa mujibu wa msemaji wa ishu hiyo, Christine Mosha ‘Seven’, Ali Kiba ataungana na mastaa wengine kutoka Afrika wakiwemo Navio (Uganda), Amani (Kenya), 2Face (Nigeria), Fally Ipupa (Congo), JK (Zambia), 4x4 (Ghana) na wengine waliopata nafasi hiyo kupitia utafiti uliofanywa na Kituo cha Televisheni cha MTV Base wa kutafuta wasanii wakali kwa nchi za Afrika.

Kabla ya safari hiyo, mwanzoni mwa wiki hii, Kiba anayeendelea kufanya vizuri na video ya wimbo wake wa Hadithi iliyoandaliwa na Mtayarishaji, Malcom akiwa katika mchakato huo wa kusepa kwa Obama alijikuta akidondokea kwenye vikwazo pale aliposhindwa kupata Viza ndani ya Ubalozi wa Marekani.

Staa huyo wa ngoma ya Usiniseme alifika katika Ubalozi huo uliopo pande za Drive In, Dar Jumatatu asubuhi kwa ajili ya kushughulikia ishu hiyo lakini aliambiwa na mmoja wa maafisa wa ubalozi huo kuwa hawezi kupata Viza kwa sababu pasipoti yake ilikuwa inakaribia kwisha muda na kwamba alitakiwa ‘kuirinyuu’ kitu ambacho alikitekeleza na kufanikiwa kuendelea na safari yake leo. ShowBiz inamtakia Kiba Kolabo njema na aiwakilishe vyema Bongo huko ughaibuni.

MWISHO MWAMPAMBA NDANI YA JAHAZI CLOUDS RADIO !!!

Friday, October 8, 2010

MSANII DIAMOND KUPIGA SHOW UK !!


Urban Pulse Creative ikishirikiana na Aset Inapenda kuwataarifu wadau wote wa Music wa bongo Flava na Hip Hop kuwa imeandaa tamasha maalum linaloitwa URBAN TOUR ambapo msanii Diamond kutoka bongo anayetamba na kibao chake cha Mbagala atakuwepo hapa ukerewere kuanzia mwezi wa November mwaka huu. Wasanii wengine ni Pamoja na First lady wa Urban Pulse Mish Ze Fyah Sis UK Artist anayetamba na single yake Freedom na I don't give a damn.

http://www.youtube.com/watch?v=CVMv053sTiY

Tamasha Hili ni kwa ajili ya kuchangia Vita Dhidi ya Malaria Afrika. Diamond ni ambassador wa Malaria Tanzania na ndiye atakekuwa akiwakilisha.
Shows Hivi zitafanyika tarehe 6th Nov Milton keynes, 12th Nov London and 27th Nov Birmingham.
Stay tune kwa habari zaidi.

Asanteni,

Urban pulse Creative.

RAISI JAKAYA KIKWETE ASHEREHEKEA SIKU YA KUZALIWA KWAKE JANA USIKU!!!


Rais Jakaya Kikwete akimlisha keki mkewe Mama Salma Kikwete usiku wa kuamkia leo,Mh Jk usiku wa kuamkia leo alikuwa anatimiza miaka 60.

Friday, October 1, 2010

NYUMBA YA MASHINDANO YA BONGO STAR SEARCH 2010 YAZINDULIWA DAR !!!


Jajim maarufu wa BSS Salama Jabir kulia akiwa na Ritah Paulsen Mkurugenzi wa Benchmark Production wakati wa uzinduzi wa nyumba ya BSS uliofanyika jana jijini Dar es salaam na kushirikisha wadau mbalimbali wa muziki. Ni wakati mwingine tena ambapo shindano la (BSS) litaibua vipaji vya vijana wa Tanzania na kuwanufaisha katika maisha yao katika shindano hili la 2010, Tangu shindano hilo lianze limeibua vipaji vya wasanii wengi kupitia shindano hilo na sasa wanafanya vizuri katika anga za muziki wa kizazi kipya Bongofleva hapa nchini

Menene wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe kushoto na Mkurugenzi wa Kampuni ya Benchmark ambayo ndiyo inaandaa shindano la Bongo Star Search BSS Ritah Paulsen wakawa katika picha ya pamoja na washiriki wa BSS wakati wa uzinduzi wa Nyumba ya BSS uliofanyika jijini Dar es salaam jana.

MWANAMUZIKI FERE GORA ATIKISA DAR JANA USIKU LEO KUTIKISA KIRUMBA MWANZA !!!

Mwanamuziki Fere Gora akilisakata Sebene na shabiki yake jukwaani.

Mwanamuziki Fere Gora akiwa na mwanadada.

Pichani ni Mwanamuziki Fere Gora akisalimia mashabiki wake pembeni yake ni Mtangazaji wa TBC 1 Ben Kinyaiya na Sofia kesy toka Africa Bambataa ya Clouds FM Radio.

Thursday, September 30, 2010

MWANAMUZIKI CHEGE CHIGUNDA ACHAGULIWA KUWANIA TUZO ZA ZUMARI !!!


Have been nominated for Nzumari Awards in the category of Best Male Artist,
the Ceremony wil b on 9
th oct@Club seafront Mombasa,
don't miss!

Wednesday, September 22, 2010

MWAKALEBELA ATIKISA IRINGA.AKUBALI YAISHE NA KUYAZIKA MAKUNDI !!


Mgombea Urais wa chama cha CCM,Mh Jakaya Kikwete akiwa na Frederick Mwakalebela kwa pamoja wakiwasalimia wananchi waliofika kwenye mkutano wa kampeni za chama hicho uliofanyika leo mjini Iringa

Wwwoooowww..!

Mgombea Urais chama cha CCM,Mh Jakaya Kikwete na Frederick Mwakalebela.

================


Frederick Mwakalebela ashangiliwa kuliko mgombea urais wa CCM, jazba ya wana Iringa dhidi ya kutemwa kwa kwake yaonyeshwa mbele ya Jakaya Kikwete, yeye aamua kupanda naye jukwaani .




Hata hivyo CCM jimbo la Iringa mjini imeweza kutumia jukwaa hilo la mgombea Urais kwa kuwataka wagombea wote walioshiriki katika kinyang’anyiro cha kura za maoni kupanda jukwaani ili kuvunja makundi huku wote wakikosa kushangiliwa zaidi ya Mwakalebela aliyeonyesha kushangiliwa kwa nguvu zote kuliko hata burudani zilizokuwepo hapo na wagombea wenzake.





Akitangaza kuvunja makundi ya kura za maoni Mwakalebela alisema kuwa kwa sasa ataelekeza nguvu zake zote kwa Mbega kama mgombea ubunge wa jimbo hilo na madiwani wote wa CCM na mgombea huyu wa urais Dr.Kikwete na kuwataka wapinzani wasimtumie kama sera zao.Picha zote kwa hisani ya Francis Godwin kutoka Iringa.

Tuesday, September 21, 2010

Sunday, September 12, 2010

GENEVIEV EMANUEL NDIYE MISS TANZANIA 2010 !!!


Ni furaha na tabasamu ya kutosha kabisa kutoka kwa binti Geneviev Emanuel pichani kutoka kitongoji cha Temeke,ambaye ndiye aliyelinyakua taji la Miss Tanzania 2010 usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City,Mwenge jijini Dar na kuhudhuriwa na watu kibao,aidha mshindi wa pili alikuwa ni mrembo kutoka Arusha Glory Mwanga na mshindi wa tatu kutoka kitongoji cha Ilala,mrembo Consolata Lukosi.

Saturday, September 11, 2010

MATUKIO MBALIMBALI WAKATI WA MECHI YA SIMBA NA AZAM FC LEO KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI JIJINI TANGA,AMBAPO SIMBA ILITOKA KIFUA MBELE KWA MABAO 2 - 1!!!


Kocha Mkuu wa Timu ya Simba Phiri akishow love kwa mashabiki wakati wa kuondoka uwanjani

Kocha wa Timu ya Taifa Jan Paulsen akiwa kwenye iliyomleta uwanjani pamoja na Afisa habari wa TFF Florian Kaijage.

K ocha mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania Jan Paulsen akishow Love ndani ya Kamera ya blog hii ya Easymen ndani ya Uwanja wa Mkwakwani.

Afisa habari wa TFF Florian Kaijage akiondoka uwanjani baada ya Mchezo baina ya Simba na Azam kuisha.

Basi la Wachezaji wa Azam Fc likiwa limepark tayari kwa safari ya kurudi Dar es Salaam baaday ya mchezo wao na Simba katika Hotel ya Central City barabara 8 jijini Tanga ambapo ndipo wachezaji hao walipofikia.

Mashabiki wa Timu ya Simba wa jijini Tanga wakimpa hongera mtoto wa Home Uhuru Suleiman akiwa kwenye gari baada ya Mechi kumalizika.

Mchezaji wa Simba akishow love na mashabiki wa Timu hiyo wakati wakitoka Uwanjani.

Basi la wachezaji wa Timu ya Azam Ndani ya Uwanja wa Mkwakwani punde tu baada ya Mechi kumalizika na Simba kutoka kifua mbele kwa Goli 2 - 1.

Basi la mashabiki wa Simba toka Dar es salaam likiondoka ndani ya Uwanja wa Mkwakwani kwa mbwembwe baada ya kupata ushindi dhidi ya Azam Fc.

Baadhi ya Mashabiki waliamua Kuingia uwanjani kupitia ukutani kutokana na Ticket za Mchezo huo kuisha mapema na uwanja kujaa na Kufungwa mida ya Saa kumi na nusu jioni.

Hii pia ilikuwa ni njia ya Kuingia uwanjani baada ya kuwa Ticket zimekwisha mapema na uwanja kufungwa.amabpo inasemekana Ticket zilitengenezwa 14,000 zote ziliisha.

Baadhi ya Mashabiki wa Azam waliotoka Dar es Salaam wakifanya vurugu mlango mkuu wa Uwanja wa Mkwakwani baada ya kuambiwa kuwa Ticket zimekwisha na hawataweza kuingia na kuona mchezo huo.
Mashabiki wengi waliotoka mikoani na wa jijini Tanga hawakuweza kuona mchezo huu kutokana na Ticket kuwa kidogo na Uwanja kujaa.hata mimi mwandishi wa Blog hii nilifika Uwanjani Saa kumi na dakika tano pamoja rafiki zangu lakini hatukuweza kuingia na kuona mchezo huu.