SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Friday, December 31, 2010

MH.UMMY ATEMBELEA TUJIKOMBOE GROUP TANGA!!!


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Bi.Ummy Ally Mwalimu kulia akipokea risala kutoka kwa Mwasisi Mshauri wa Shirika lisilo la kiserikali la Tujikomboe Group Bw.Shamsi Mhina ,Shirika hilo lenye makao yake Ngamiani Kusini Tanga linalojishughulisha na masuala ya kutetea haki za watoto,Maendeleo ya Jamii(Picha na Benedict Kaguo)

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Bi.Ummy Ally Mwalimu (katikati asiye na kilemba) akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Tujikomboe Group alipowatembelea jana,kulia ni Bw.Shamshi Mhina Mwasisi na Mshauri wa Shirika hilo,kushoto ni Bi Chiku Athumani Mratibu wa Shirika hilo Tanga,walioko nyuma ni Afisa Tawala Bi.Mariam Amiri na Mwanaisha Issa Msaidizi wa Ofisi,Naibu Waziri alitembelea kujua shughuli za asasi hiyo(Picha na Benedict Kaguo)

Thursday, December 23, 2010

WADAU NAWATAKIA SIKUU NJEMA YA X-MASS !! NITAKUWA KIMYA KIDOGO MPAKA BAADA YA X-MASS!!


Mimi Director wa Blog (Pashua)hii ya Eazymen nawatakia wadau wote Heri na fanaka katika kusherehekea sikukuu ya X-Mass.
Nitakuwa kimya mpaka baada ya sikuu kwa hiyo wadau tuwiane radhi.

PROF,NDULU PRESENTED THE TANZANIAN SHILING CURRENCY NOTE TO PRESIDENT KIKWETE TODAY!!!


The Governor of Bank of Tanzania Prof.Benno Ndulu today presented the new Tanzanian shilling currency note to President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete at Dar es Salaam State House this afternoon. The New Currency Note will be in circulation from January next year and they will be used alongside with the current bank notes. In the Picture The Central Bank Governor(left) Prof.Benno Ndulu presents a special album with new Tanzanian shilling currency notes to President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete while the Minister for Finance Dr.Mustafa Mkullo,(right) looks on.

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete examines special security features in some of the new banknotes presented to him by the Governor of the Central Bank Prof. Benno Ndulu at Dar es Salaam State House this evening.

A senior Principal bank Officer, from the Central Bank’s Directorate of Banking, Mr.Juma Hassan Kimwaga shows President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete, special security features in the new Tanzanian shilling currency notes at Dar es Salaam State House this evening.(photos by Freddy Maro).

TID KUZINDUA ALBUM YA SIFAI DESEMBA 28,2010.CLUB BILLICANAS!!

WAZIRI NUNDU AWASHUKIA WATENDAJI TPA WANAOTAKA UTAJIRI WA HARAKAHARAKA KWA NJIA YA RUSHWA!!!


Waziri wa uchukuzi Omari Rashid Nundu (kushoto)na Naibu wa waziri wa wizara hiyo Mhandisi Athumani Mfutakamba(wa pili kushoto),wakimsikiliza kwa makini meneja wa kitengo cha kuhudumia makontena bandarini(TICTS),Donald Talawa(kulia)akiwaeleza namna kitengo hicho kinavyofanya kazi zake,alipotembelea kituo cha kitengo hicho kilichopo Ubungo jijini Daresalaam.

Waziri wa uchukuzi Omari Rashidi Nundu (kushoto)akikagua kituo cha kuhudumia makontena cha kampuni ya AMI,alipofanya ziara ya kukagua shughuli zinazohusiana na mamlaka ya bandari Tanzania (TPA)jijini Daresalaam.wapili ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo Grant Lendrum.

Mawakala wa kutoa magari bandarini wakitoa madukuduku yao mbele ya waziri Nundu wakati wa ziara hiyo.

Sunday, December 19, 2010

RATIBA YA MAZISHI YA NGULI WA DRUMS ABUU SEMHANDO,BABA DIANA !!!


Waliosimama..Remmy Ongala, Abuu Semhando, Kasaloo Kyanga, Fan Fan

Ratiba ya Mazishi ya mwanamuziki na na meneja wa Bendi ya African Stars-Twanga Pepeta Marehemu Abou Ally Semhando “Baba Diana”
· Jumamosi ndugu na jamaa walikusanyika nyumbani kwa marehemu, Mwananyamala Kisiwani(Ngilangwa) kwa ajili ya kutoa pole na kuwafariji wafiwa.

· Leo Jumapili 19/12-Saa11 baada ya Swala ya alfajiri katika msikiti wa Muhimbili, waombolezaji kuingia katika magari na kuelekea kijiji cha Kibanda, Muheza tayari kwa mazishi.

· Mara baada ya chakula cha mchana mwili kupelekwa msikiti wa Muheza nabaada ya swala mwili kupelekwa makaburini kwa maziko.

· Waombolezaji watarejea Dar es Salaam baada ya maziko.

Hakika Msiba wa Abou unaumiza sana

1. Jumamosi ni siku aliyokuwa amuoze binti yake wa kwanza
2. Alikuwa ameuandikia uongozi wa Bendi kuwa umpe likizo ya mwezi kwani alitaka asiweko katika jukwaa kwa kipindi. Ni mara ya kwanza yeye kuandika barua ya kuomba likizo
3. Katika simu yake ringtone aliyoiweka ni ya wimbo wa Njohole Jazz Band- bendi hii wanamuziki wake karibu wote walikufa pamoja katika ajali mbaya ya gari.


4. Alikuwa mpiga drum wa Dk. Remmy Ongala enzi za Super Matimila na mtindo wao wa Talakaka mwaka 1981

-John Kitime

Tuesday, December 7, 2010

PETER MSECHU AMBAYE NI MSHINDI WA PILI TUSKER PROJECT FAME4 AWASILI JIJINI DAR LEO MCHANA NA KUPOKEWA KWA SHANGWE !!!


Mshindi wa pili wa Tusker project fame4 kutoka Tanzania Peter Msechu akiwapungia mkono baadhi ya mashabiki wake waliojitokeza kumpokea katika uwanja wa ndege wa mwalimu Nyerere Dar leo mchana.

Peter Msechu akiwa na mchumba wake anayeitwa Amalis katika picha ya Pozi.

Blog hii ya Esymen pamoja na studio ya muziki ya blog hii ijulikanayo kama 2MORROW RECORDZ iliyopo jijini Tanga ambapo tuliwahi kufanya baadhi ya kazi pamoja na wewe tunakupongeza kwa ushindi huo ulioupata.

Friday, December 3, 2010

MH UMMY MWALIMU AANZA KAZI KWA KUWA MGENI RASMI SHEREHE ZA WALEMAVU !!!


Mhe. Ummy Ali Mwalimu akimkabidhi Mtoto mwenye Ulemavu wa Miguu Baiskeli ya kumwezesha kutembea.Hii ilikuwa ni wakati wa Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu iliyoadhimishwa kitaifa huko Mkuranga. Jumla ya Baiskeli 50 Zimetolewa kwa Ajili ya kuwasaidia Watu wenye Ulemavu Wilayani humo.

Mhe.Ummy Ali Mwalimu akisoma Hotuba yake wakati
Siku hii ya Walemavu huko Mkuranga.


Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii, wanawake na watoto, Mhe.Ummy Ali Mwalimu,Mhe.Al-Shymaar wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Henry Orauya( Kulia) pamoja na Viongozi Wakuu wa Wilaya hiyo, mara baada ya kuwasili Wilayani hapo.
Sisi wananchi wenzako wa Tanga tunajivunia kwa Mh Raisi kukuchagua kuwa Naibu waziri na tunakutakia kila la heri katika kazi zako za Unaibu Waziri na katu usiutupe mkoa wako wa Tanga.Tanga Oyee!!!:-)

Thursday, December 2, 2010

WAZIRI MAGUFULI AMTIMUA KAZI CEO WA TANROADS !!


Waziri wa ujenzi Dk John Magufuli ameanza kazi kwa maamuzi magumu kwa kumfukuza kazi mtendaji mkuu(CEO)wa wakala wa barabara Tanzania(TANROAD)Ndg Ephraim Mrema.
Habari za uhakika ambazo Nipashe limezipata kutoka vyanzo vya kuaminika zianaeleza kwamba Magufuli alifanya uamuzi huo jana.
Vyanzo hivyo havikueleza sababu ya kumtimua mrema zaidi ya kusema uamuzi huo unaanza mara moja.
Habari zaidi zinasema kuwa Dk Magufuli alimtaka Mrema kukabidhi ofisi jana mchana na nafasi yake inashikiliwa kwa muda na mkurugenzi wa barabara za vijijini Patrik Mfugale.
Hata hivyo Nipashe lilimtafuta Dk Magufuli jana usiku ili kuthibisha uamuzi huo lakini simu yake ya kiganjani ilikuwa imezimwa.habari kwa hisani ya nipashe.

Wednesday, December 1, 2010

DR GHARIB BILAL AADHIMISHA SIKU YA UKIMWI KITAIFA MKOANI MOROGORO !!!


Makamu wa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Ghalib Bila,akikabidhi cheti na kikombe kwa muwakilishi wa shirika la champion kwa ushiriki wake bora katika maonesho ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyoadhimishwa kitaifa mkoani Morogoro leo.

wasanii wa kundi la vichekesho la Orijino komedi wakiwaburudisha wananchi wa mkoa wa Morogoro waliohudhuria maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri.

Makamu wa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Mohamed Ghalib Bilali akilihutubia taifa kwenye maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yaliyofanyika kitaifa katika uwanja wa jamhuri mkoani Morogoro.