SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Sunday, October 24, 2010

MWANAMUZIKI ALLY KIBA AZIDI KUNG'AA KIMATAIFA


Ali Kiba Kusepa Marekani, kupiga kolabo na R.Kelly
-------

Kutoka ndani ya mradi wa muziki wa kizazi kipya, msanii Ali Kiba anatarajia kuondoka leo kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya kugonga ngoma ya pamoja na baadhi ya mastaa wa Afrika, kabla ya kufanya kolabo na staa wa kimataifa, Robert Kelly wa pande hizo.

Kwa mujibu wa msemaji wa ishu hiyo, Christine Mosha ‘Seven’, Ali Kiba ataungana na mastaa wengine kutoka Afrika wakiwemo Navio (Uganda), Amani (Kenya), 2Face (Nigeria), Fally Ipupa (Congo), JK (Zambia), 4x4 (Ghana) na wengine waliopata nafasi hiyo kupitia utafiti uliofanywa na Kituo cha Televisheni cha MTV Base wa kutafuta wasanii wakali kwa nchi za Afrika.

Kabla ya safari hiyo, mwanzoni mwa wiki hii, Kiba anayeendelea kufanya vizuri na video ya wimbo wake wa Hadithi iliyoandaliwa na Mtayarishaji, Malcom akiwa katika mchakato huo wa kusepa kwa Obama alijikuta akidondokea kwenye vikwazo pale aliposhindwa kupata Viza ndani ya Ubalozi wa Marekani.

Staa huyo wa ngoma ya Usiniseme alifika katika Ubalozi huo uliopo pande za Drive In, Dar Jumatatu asubuhi kwa ajili ya kushughulikia ishu hiyo lakini aliambiwa na mmoja wa maafisa wa ubalozi huo kuwa hawezi kupata Viza kwa sababu pasipoti yake ilikuwa inakaribia kwisha muda na kwamba alitakiwa ‘kuirinyuu’ kitu ambacho alikitekeleza na kufanikiwa kuendelea na safari yake leo. ShowBiz inamtakia Kiba Kolabo njema na aiwakilishe vyema Bongo huko ughaibuni.

No comments:

Post a Comment