SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Friday, July 16, 2010

UKWELI KUHUSU WIMBO WA KIDUMU NITAFANYA Ft LADY JAYDEE TOKA KWA PRODUCER HERMY B !!!


Ngoja nitoe ukweli wa huu wimbo. Kidum alipokuja Dar aliamua kumtafuta Hermy B ambae alikutana nae Project FAME kule Nairobi.

Wakakutana na kufanya kazi pamoja..katika maana ya kwamba mziki huu uliundwa na Hermy na Kidumu akitoa melodies. Drum Patern Yote ni Ya hermy. Kidum aliporudi kule Nairobi akakutana na Rkay(jamaa anaetengeneza mziki wa Wahu examples Sweetlove, Runin Low) madhumuni ni kutengeneza video ya wimbo huu.

Cha ajabu Rkay akamtengeneza Kidum mpaka akakubali kurekodi upyaa wimbo huo. Rkay alikopi kila kitu ila akabadili sauti tofauti kidooogo, ila kisheria alibeba Idea ya kisanii ya Hermy kama ilivo. yote haya yalifanyika bila kuomba ruhusa wala kumpa taarifa Hermy.

Muda ulipofika Hermy alitoa huo mziki kwa radio stesheni, na kidumu alikimbilia kuomba wasiucheze huo wasubiri ule wa Rkay..alipoulizwa huu una tatizo lipi alishindwa kujieleza na akagundulika hana mantiki zaidi ya Ubaguzi wa sanaa tu. Stesheni flani flani wakakubali kuupokea na kuucheza huu wa kwetu Tanzania. Hermy hakutaka kuongea chochote kile mpaka alipoona wimbo huo wa Rkay ukichezwa na upo kwa video aliyopiga Rkay kwa sasa.

Mwenye maskio na aliyeskia wimbo huu mara ya kwanza atajua tu huu uliopo kwenye video ni tofauti na vyombo vimepunguzwa, sio kwamba Rkay hajui kutengeneza muziki, ila alikua akijaribu kujitofautisha sana na Hermy na amejikuta akiharibu kiasi flani sanaa hiyo.

Ninachoomba ni kwamba watanzania tuendelee kushikamana na kupeana suport kwenye wizi wa sanaa kama huu. Tuwe na cha kujivunia kwa watengeneza mziki wetu.
Asalaamu!

No comments:

Post a Comment