SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Wednesday, July 21, 2010

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) CHAMTEUA DR,WILBROD SLAA KUWA MGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA CHADEMA !!!


Kutoka kushoto ni mwenyekiti wa chama hicho Nd Freeman Mbowe,Katikati ni Mh Dr Wilbrod Slaa na kulia ni Mh Zitto Kabwe.hapa ni katika moja ya vikao vyao vya chama.


BAADA ya kutafakari na kujaribu kushawishi watu mbalimbali, hatimaye Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilikutana kutafuta wa kukibebea bendera katika kinyang’anyiro cha urais.

Hata hivyo, jina la Katibu Mkuu wake Dk. Wilbroad Slaa, ndilo pekee ambalo hadi jana lilikuwa linatajwa kuombwa rasmi na Chama hicho ili abebe bendera hiyo.

Kamati Kuu ya Chadema ilikuwa na kikao ambacho pamoja na ajenda zingine, moja ya ajenda hizo, ilikuwa ni kuteua jina la mgombea urais ambaye atachuana na wagombea wa CUF, CCM na TLP.

“Ninachoweza kukwambia ni kwamba Kamati Kuu imemwomba Dk. Slaa awe mgombea urais wa Chadema na amekubali,” alisema mpasha habari wetu ambaye anahudhuria vikao vya chama hicho vinavyofanyika katika hoteli moja ya Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment