SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Saturday, May 7, 2011

MWANAIDI HASSANI AIBUKA MWANAMICHEZO BORA WA JUMLA TUZO ZA TASWA,RAISI MSTAAFU MH MKAPA APEWA TUZO YA HESHIMA!!


Mgeni rasmi,Makamu wa rais, Dk Gharib Bilal akimkabidhi tuzo kwa mwanamichezo wa jumala Bi Mwanaidi Hassani anayecheza mchezo wa Netball katika timu ya JKT Mbweni.Mwanaidi ndie aliyejinyakulia gari aina ya Toyota GX 100,iliyotolewa na kampuni ya Bia ya Serengeti ambao ndio waliokuwa wadhamimi wakuu wa tuzo hizo za kumsaka mwanamichezo bora wa mwaka zilizoratibiwa na TASWA,kushoto ni waziri wa Vijana,Habari,utamaduni na michezo Mh Emanuel Nchimbi akishuhudia tukio hilo.


Raisi mstaafu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh Benjamini William Mkapa akipokea tuzo yake ya Heshima kutoka kwa Makamu wa Raisi Dk,Gharib Bilali.
Chama cha waandishi wa habari za michezo (TASWA)kimempa Mzee Mkapa tuzo hiyo maalumu ya Heshima kutokana na mchango wake katika michezo hasa ujenzi wa uwanja mpya wa Taifa. Mzee Mkapa amesisitiza uwanja huo uendelee kutunzwa vyema ili nchi yetu iweze kuwa na kumbukumbu na urithi kwa vizazi vijavyo.
Pichani kulia ni mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni ya Serengeti (SBL)Teddy Mapunda.Katika utoaji wa tuzo hizo mchezaji wa jumla ni Mwanaidi Hassani anayechezea timu ya Netball ya JKT MBWENI.

No comments:

Post a Comment