SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Monday, February 28, 2011

ROMA kuwasha moto ndani ya La Grande Lacasa Chica Tanga !!!



Msanii wa Kizazi kipya Ibrahim Mussa a.k.a Roma anatarajia kuwasha moto mjini Tanga kuwashukuru wakazi wa mkoa huo kwa kuweza kumuunga mkono katika kazi yake ya sanaa ambayo amekuwa akiifanya.

Akizungumza na blog hii, mratibu wa tamasha hilo lililopewa jina la 'Narudi Nyumbani Tanga, Bw. Nickson Amos alisema kuwa litafanyika katika ukumbi wa La Gland la Casa chica Ijumaa ya tarehe 4.03.2011.

"Kweli Roma atafanya tamasha lake binafsi ambalo anatarajia kusindikizwa na Belle 9, Young D pamoja na Dogo Janja hivyo wakazi wa Tanga waje kwa wingi kumuunga mkono.

Aliongeza kuwa lengo la tamasha hilo kuwashukuru wakazi wa Tanga kwa kuweza kumuunga mkono tokea ameanza kazi zake.

Karibu sana Home Roma.

Wednesday, February 23, 2011

SEMINA YA WASANII WATEULE WA TUZO ZA KILIMANJARO TANZANIA MUSIC AWARDS YAFANYIKA LEO JIJINI DAR !!!!


Meneja wa Kinywaji cha Kilimanjaro Premium Lager,George Kavishe akifafanua jambo leo jioni kwenye Semina ya wateule wa Tuzo za muziki Tanzania (Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2011)ndani ya moja ya ukumbi wa Hoteli ya Paradise.

FID Q na F.A ndani ya Semina ya Kili Tanzania Music Awards.

Mwanamuziki Mkongwe wa Raggae hapa nchini,Innocent akitoa ufafanuzi kwa wasanii wa muziki waliofika kwenye semina ya wateule wa Tuzo za muziki Tanzania.(Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2011.) ndani ya moja ya ukumbi wa Hoteli ya Paradise.

Muwakilishi wa Kampuni ya mahesabu ya Innovate ambao watasimamia upigaji/kuhesabu kura katika Tuzo hizo Bw, Leornad Chacha akifafanua jambo mbele ya wasanii wateule wa Tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards namna ya upigaji kura wa Tuzo hizo zitakazofanyika March 26. 2011.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ajulikane kwa Jina la Shaa akiuliza swali katika semina hiyo.

Mwanamuziki Mkongwe wa Taarabu,Hadija Kopa akiuliza swali kwa wahusika wa Tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2011.




KUNDI LA MUZIKI WA BONGO FLEVA EAZYMEN CREW AMBALO PIA LINAMILIKI BLOG HII NA STUDIO YA KUREKODI JIJINI TANGA MAARUFU KAMA 2MORROW RECORDZ !!!!




Kundi hili la Muziki la EAZY MEN CREW linaundwa na wasanii 5 ambao ni mimi Editor wa Blog hii maarufu kama Pashua,Johnior,Mido Man,Voicer na K square.

Saturday, February 19, 2011

DUH, HUYU DOGO NOMA !!!!

RAISI WA ZANZIBAR DR ALI SHEIN AWAJULIA HALI WAATHIRIKA WA MABOMU YA GONGO LA MBOTO !!!


Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein akizungumza na wabunge wa mkoa wa Dar es salaam nje ya wodi ya Muhimbili baada ya kuwajulia hali waathirika wa mabomu ya Gongo la Mboto jana jijini Dar es Salaam.

Thursday, February 17, 2011

RAIS JAKAYA KIKWETE ATEMBELEA ENEO LA TUKIO KULIPOLIPUKA MABOMU NA KUWAFARIJI WANANCHI !!!


Amiri Jeshi mkuu Raisi Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na wahandishi wa habari baada ya kukagua eneo la tukio mapema leo katika kambi ya jeshi la JWTZ Gongo la Mboto yalikolipuka mabomu hayo.

Waziri wa Ulinzi Dr. Hussein Mwinyi akizungumza na mkuu wa JWTZ General Davis Mwamunyange na mnadhimu wa jeshi hilo mapema leo mara baada ya Raisi kuondoka eneo la tukio.

Majeruhi aliyefikishwa Hospitali ya Temeke akiwa hoi akisaidiwa.

Baadhi ya majeruhi wakiwa katika hospitali ya Temeke wakipatiwa huduma ya matibabu.

Nyumba iliyoharibiwa vibaya na mabomu hayo yaliyolipuka katika kambi ya jeshi la wananchi Gongo la Mboto jijini Daresalaam.

HALI ILIVYOKUWA LEO KWA WAHANGA WA MABOMU YA GONGO LA MBOTO NDANI YA UWANJA WA UHURU JIJINI DAR !!!


Sehemu ya wahanga wa Mabomu ya Gongo la Mboto wakiwa ndani ya Uwanja wa Uhuru jijini Dar wakisubiria kujua nini kinaendelea juu yao.

Baadhi ya watoto wakiendelea kuletwa katika uwanja huo wa Uhuru kwa ajili ya mapumziko na kama kuna ndugu aweze kuwatambua.

Wengine walikaa nje ya Uwanja wa Uhuru kupumzika na kupata vivuli vya miti kutokana na kutolala usiku wa kuamkia leo kwa hali ya milipuko ya mabomu iliyotokea maeneo ya Gongo la Mboto katika maghala ya silaha ndani ya kambi ya jeshi la wananchi (JWTZ)

Mtoto Gerald Samson ambaye ni mmoja wa wahanga akiwa na majeraha usoni mara baada ya kuumia wakati akijaribu kutaka kujinusuru na milipuko hiyo jana usiku.

Hawa ni watoto waliookotwa huko Gongo la Mboto wakiwa peke yao kutokana na wazazi wao kukimbilia sehemu zisizojulikana kutokana na mabomu yaliyokuwa yakilipuka usiku wa kuamkia leo katika kambi ya jeshi la wananchi (JWTZ)huko Gongo la mboto.

Bw Salum Madaba wa Ofisi ya mkuu wa Mkoa pamoja na mwalimu Kiondo kutoka shule ya msingi Tandika wakimnywesha maziwa mmoja wa watoto waliopo katika uwanja wa Uhuru jijini Dar.ambapo haikufahamika wazazi wake wapo wapi mpaka leo hii.

Afisa Msalaba Mwekundu mama Jane Lweikiza akiwa amembeba mtoto aliyekutwa maeneo ya Sitaki Shari Ukonga mchana huu kutokana na kutojulikana walipo wazazi wake mara baada ya kutokea kwa milipuko ya mabomu katika kambi ya jeshi la Wananchi (JWTZ) Gongo la mboto usiku wa kuamkia leo.

Watu wa msalaba mwekundu wakishusha maji ya kunywa kwa ajili ya wahanga hao waliopo ndani ya uwanja wa Uhuru jijini Dar,

VODACOM FOUNDATION KUSAIDIA WAHANGA WA MABOMU YA GONGO LA MBOTO !!!!


Mkurugenzi wa mahusiano na Vodacom Foundation Bi Mwanvita Makamba ameviambia vyombo vya habari kwamba.
Kampuni yake kupitia mfuko wa kusaidia jamii wa Vodacom Foundation umeguswa na janga la milipuko ya mabomu yaliyotokea katika kambi ya jeshi ya Gongolamboto jijini Dar es salaam na hivyo kufanya maamuzi ya haraka kama yafuatayo:
1.Kufungua tena namba yao ya maafa ili kuruhusu watanzania ambao wangependa kuchangia wenzao kufanya hivyo kwa kutuma ujumbe mfupi kwenda 15599 kupitia mitandao yote.Ujumbe huu utatozwa shilingi 1,000 na pesa zote zitaenda kwenye tume ya maafa ya serikali ili kuweza kununua vitu vya dharura vya wahanga.Red alert itawasha kesho Ijumaa tarehe 18.
2.Vodacom Foundation itatoa chakula na vinywaji kwa siku nzima ya Ijumaa kwa wahanga 1000 waliopo uwanja wa Taifa wengi wao wakiwa ni watoto.
3.Pia Vodacom Foundation imetoa namba za simu kwa timu ya Clouds iliyoanzisha kituo cha habari na matukio katika shule ya msingi Mzambarauni Ukonga. Namba hizi zinatumika bure kupiga na kutoa taarifa kama umepotelewa na ndugu au jamaa na pia kutoa taarifa zaidi kuhusu maafa ambayo hayajulikani ili taarifa ziende kwa wahusika.Namba hizo ni 0767111401,0767 111402, 0767 111403.
4.Pampja na kuwawezesha watanzania kutuma michango yao kupitia ujumbe mfupi.Vodacom Foundation pia inakusanya misaada ya chakula na maji na vifaa mbalimbali katika ofisi zao zilizopo Mlimani City kwa watu ambao hawajui waipeleke wapi.Misaada hiyo itakabidhiwa kwa Redcross ambao wanawahudumia wahanga waliopo Uwanja wa Taifa na sehemu mbalimbali.

Tuesday, February 8, 2011

C PWAA KUZINDUA ALBUM CLUB MAISHA FEB 13th !!!!

MKUU WA MKOA WA TANGA AZINDUA KAMPENI ZA WEKA TANGA SAFI KWA USHIRIKIANO NA AURORA SECURITY LEO JIJINI TANGA!!!


Mkurugenzi wa Aurora Security Akitoa shukrani zake mbele ya mkuu wa Mkoa wa Tanga Meja Mstaafu Said Said Kalembo kufuatia kampuni yake ya Aurora kutoa msaada wa Mapipa ya kuhifadhia takataka ambayo yatatumika katika maeneo mbali mbali ya jiji la Tanga. Hafla hii imefanyika katika viwanja vya Tangamano jijini Tanga na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa serikali na watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga.
Wageni mbalimbali waalikwa katika Uzinduzi huo ambao unaojulikana kama Weka Tanga Safi.

Mapipa ya Kuhifadhia Taka ambayo yametolewa kwa msaada wa Kampuni ya Aurora Security ambayo yatatumika katika maeneo mbali mbali ya jiji la Tanga.

Wageni mbalimbali pamoja na wafanyakazi wa Idara ya Afya katika Halmashauri ya Jiji la Tanga wakifuatilia kwa makini Uzinduzi huo uliofanyika katika viwanja vya Tangamano jijini Tanga.

Wasanii wa kikundi cha Town Boyz wakitoa burudani katika uzinduzi huo wa weka Tanga Safi leo katika viwanja vya Tangamano jijini Tanga.

Saturday, February 5, 2011

KOMRED ALI CHOKI AKOMBA VIFAA VYA TWANGA PEPETA !!!


Kiongozi wa bendi ya Muziki wa Dansi ya EXTRA BONGO,Ally Choki(katikati mbele)akiwa na wanamuziki wapya kutoka bendi ya African Stars,Twanga Pepeta,wakati wa mkutano wa waandishi na habari,alipokuwa akiwatambuliasha wanamuziki hao kwa waandishi wa habari.
Wanamuziki hao waliojiunga na bendi hiyo ni,Rogert Hega Katapiler,Rapa wa bendi hiyo Soul John (Furguson)ambaye aliibuka katika bendi hiyo hiyo ya Extra Bongo na kiongozi wa wanenguaji wa Twanga Super Nyamwela,Danger Boy na Otilia.

MAADHIMISHO YA MIAKA 34 YA KUZALIWA KWA CCM YAFANA MJINI DODOMA LEO!!!


Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM)Raisi Jakaya Mrisho Kikwete akiwashukuru wanachama wa CCM walioshiriki matembezi maalum ya maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa CCM Mjini Dodoma leo asubuhi.(Picha na Fredi Maro).

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Raisi Jakaya Kikete (wa tatu kushoto) na mkewe Salma kikwete (wa nne kushoto)wakiwaongoza wanachama wa CCM wa mkoa wa Dodoma katika matembezi ya sherehe za maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa CCM mnamo mwaka 1977.Kulia ni Katibu mkuu wa CCM Yusuph Makamba na wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Dodoma.

Baadhi ya wanachama wa CCM wa mkoa wa Dodoma wakishiriki matembezi maalum ya kuadhimisha miaka 34 ya kuzaliwa chama cha mapinduzi.Matembezi hayo yalianza katika Ofisi za CCM Mkoa na kuishia katika bustani ya mwalimu nyerere mjini Dodoma.

ALI KIBA AFANYA VIDEO YA WIMBO WAKE WA DUSHELELE!!!



Mtu mzima Ally Kiba juzi kati alikuwa anashoot video yake mpya na kampuni ya GRM huko bush, Ally alikuwa akishoot wimbo wake mpya unaoitwa DUSHELELE.
Fore more picture visit
http://www.grmproductiontz.blogspot.com

DUH HII HAIJAKAA POA!!!


Kwenye mtandao wa Facebook mtu mzima Jaffarai ameendelea na maneno yake na leo ametoboa hivi daaah:


"Nimeachana na Shyrose Bhanji (kicheche mzee) baada ya kugundua km anatoka kimapenzi na mr 2... ni aibu sana kwa mwanamke mwenye miaka 42 kua kicheche kiac hicho!!!! nilitegemea mtu km mr 2 angeanza kufanya harakati ktk mziki wetu lkn harakati zake zimehamia kwenya mapenzi na madem wa wasanii wenzake... ni aibu kubwa sana"

Wednesday, February 2, 2011

JANUARY MKAMBA (MB) AZINDUA HUDUMA YA BURE YA SMS KUWASILIANA NAYE!!!

o
Mfumo wa mawasiliano kwa njia ya SMS kati ya wananchi wa Bumbuli na mbunge wao Ndg Januari Makamba yamezinduliwa tarehe 29 January kwenye semina elekezi aliyoitisha mbunge huyo kwa viongozi na watendaji wa vijiji na kata wapatao 250 wa jimbo la Bumbuli.
Mfumo huo utaanza kutumika kanzia February 10 mwaka huu wa 2011 baada ya kipindi cha elimu kwa wananchi juu ya matumizi ya huduma hii kukamilika.

Zaidi tembelea www.januarymakamba.com

Tuesday, February 1, 2011

MATUKIO KATIKA PICHA LEO JIJINI TANGA !!!


Soko huria la Nguo jijini Tanga maarufu kama Tangamano siku ya leo Jumanne.ambapo soko hili hufanyika kila siku za Jumanne, Alhamisi na Jumamosi.


Leo mchana mandhari ya kipita shoto cha Mabanda ya Papa jijini Tanga.hapa ndipo njia ya kwenda wilaya ya Pangani inapoanzia.

JIONI YA LEO MITAA YA HOTNET CAFE KARIBU NA 4WAYS TANGA!!!