SIKILIZA NYIMBO ZA EASYMEN HAPA:


Electronic Press Kit
Quantcast

Tazama Small Interview ya Easymen Studio Hapa:

Saturday, June 11, 2011

VIONGOZI WA SERIKALI YA KATA YA NGUVUMALI PAMOJA NA WAZAZI WABARIKI ZIARA YA VIJANA 10 WA KITUO CHA VIJANA NGUVUMALI KWENDA NCHINI HUNGARY !!!


Leo katika ofisi zetu za kituo cha vijana Nguvumali tulifanya mkutano uliowahusisha wazazi wenye watoto amabo ni wanachama wa kituo,vijana wenyewe na Uongozi wa kata ya Nguvumali ambapo kituo hiki cha vijana Nguvumali kipo.Lengo na madhumuni ya mkutano huu ni kuweza kufahamiana wazazi na viongozi wa kituo na serikali,pia kupokea taarifa ya Kituo na viongozi pamoja na wazazi kutoa nasaha zao kwa vijana wa kituo hiki ambao watashiriki katika ziara ya kubadilishana uzoefu Itakayofanyika tarehe 15/06/2011 ambapo vijana 5 kutoka kituo hiki watasafiri kwenda nchini Hungary kwa muda wa mwezi mmoja kufanya shughuli za kujitolea na kituo kingine cha vijana kilichopo nchini humo.group lingine la vijana 5 litasafiri tarehe 25/07/2011 nalo pia litakaa nchini Hunagry kwa muda wa mwezi 1.Pichani ni meza Kuu,toka kushoto ni Afisa maendelo ya jamii kata ya Nguvumali,Mtendaji kata wa Nguvumali,Meneja wa kituo,Mh Diwani wa kata ya Nguvumali na Katibu wa kituo.

Wazazi pamoja na wageni waalikwa wakisiliza kwa makini hotuba ya mgeni rasmi Mh Diwani wa kata ya nguvumali aliyoitoa katika mkutano huo.

Wazazi upande wa kinamama wakisikiliza kwa makini.


Wazazi pamoja na vijana wao ambao ni wanachama wa kituo hiki wakisiliza kwa makini wakati mkutano huu ukiendelea leo katika kituo cha vijana Nguvumali.

Mimi Pashua nikipokea Hati ya Bima ya Afya ya Kimataifa toka kwa mgeni rasmi ambaye ni Mh Diwani wa Kata ya Nguvumali ambayo itanisaidia kama nitapata matatizo ya kiafya kwa kipindi chote cha mwezi 1 nitakachokaa nchi Hungary.

Kijana John Omary akipokea hati ya bima ya afya toka kwa mgeni rasmi.

Katibu wa kituo Kassam Kassimila akipokea hati ya bima ya Afya toka kwa mgeni ambapo yeye ni miongoni mwa vijana 10 watakaoshiriki katika safari hiyo.

Kijana Linus Lucian ambaye pia ni mkuu wa nidhamu wa kituo akipokea hati ya bima ya toka kwa mgeni rasmi.

MWIZI APONEA CHUPUCHUPU KUUAWA NA WANANCHI BAADA YA KUIBA VIATU MSIKITINI !!!

Umati wa watu ukiwa umezingira msikiti wa Mabawa kungojea mwizi aliyekatwa msikitini hapo akiiba Makobazi.Uongozi wa msikiti huo ilibidi kumficha mwizi huyo ndani kutokana na wananchi wenye hasira kali kutaka kumpiga hadi kumuua.baada ya mvutano mkali kati ya wananchi waliotaka mwizi huyo atolewe ili wamuadhibu uongozi wa msikiti uliliarif jeshi la polisi ili kuleta ulinzi na kumuondoa mwizi huyo akiwa salama.mara ya kwanza walifika polisi 4 ambao pia wananchi waliwazidi nguvu jeshi la polisi lilileta kikosi cha kutuliza ghasia FFU ambapo walifanikiwa kuwadhibiti wananchi na kumtoa mwizi huyo kutoka kwenye msikiti na kumpeleka Kituoni.


Gari la polisi kikosi cha kutuliza ghasia likiondoka katika msikiti huo maeneo ya Mabawa na mwizi huyo akiwa ndani ya gari hilo.


Gari hilo la polisi likitokomea na wananchi wasijue wafanye nini.

SIKU TULIPOMUAGA MFANYAKAZI MWENZETU OFISINI KWA KUWA ANAKWENDA KUENDELEA NA MASOMO !!!


Mfanyakazi mwenzetu kazini aliyevaa Kitenge akipata iliyondaliwa maalum kwa ajili ya kumuaga kwa kuwa anakwenda kuendelea na masomo yake ya juu.ilikuwa ni siku ya huzuni sana kwani tulimzoea sana.


Pichani keki hiyo yenye maneno ya kwamba KILA LA HERI SHAMSA.


Pichani mkurugenzi wetu mama Ruth akimpa Zawadi ya kitenge chenye nembo ya kampuni yetu kama ukumbusho kwa mema aliyoyatenda kwenye kampuni.
Hapa mimi Pashua niliombwa kuburudisha wafanyakazi wenzangu kwenye Party hii ya kumuaga mwenzetu kwa kuimba wimbo niliomshirikisha mfanyakazi mwenzangu pia pichani anaitwa Mocky wimbo unaitwa UNFORGETABLE.

Zoezi la Kuburudisha likiendelea.